Pages

Thursday, May 2, 2013

ASA MBIONI KUTOA MBEGU MPYA YA ALIZETI (BOFYA KUTOA MAONI)

 


Ni taarifa njema kutoka kwa wakala wa mbegu wa serikali (ASA) kuwa iko mbioni kutangaza mbegu mpya ya alizeti iliyogunduliwa juzi na moja ya vituo vyake vya utafiti. Akitoa taarifa hizo katika mkutano wa shirika la maendeleo lisilo la kiserikali la RLDC katika mkutano na washirika uliofanyika mkoani Singida wiki iliyopita, Mkurugenzi wa Masoko wa ASA Mr. Kawamala alisema mbegu hiyo inauwezo mkubwa kuliko Record ambayo kwa sasa ndiyo inayoongoza nchini. Mbegu hiyo vile vile inauwezo mkubwa wa kuvumilia ukame. Bado chanzo chetu kinatafuta taarifa zaidi juu ya mbegu hii na itawajuza wadau pindi taarifa hizo zitakapotufikia. Kama mdau una taarifa yoyote karibu utujuze.


1 comment:

  1. Pamoja na kuwapongeza ASA watuambie mbegu hiyo itatoka lini?

    ReplyDelete