Ni taarifa njema kutoka kwa wakala
wa mbegu wa serikali (ASA) kuwa iko mbioni kutangaza mbegu mpya ya alizeti
iliyogunduliwa juzi na moja ya vituo vyake vya utafiti. Akitoa taarifa hizo
katika mkutano wa shirika la maendeleo lisilo la kiserikali la RLDC katika
mkutano na washirika uliofanyika mkoani Singida wiki iliyopita, Mkurugenzi wa
Masoko wa ASA Mr. Kawamala alisema mbegu hiyo inauwezo mkubwa kuliko Record
ambayo kwa sasa ndiyo inayoongoza nchini. Mbegu hiyo vile vile inauwezo mkubwa
wa kuvumilia ukame. Bado chanzo chetu kinatafuta taarifa zaidi juu ya mbegu hii
na itawajuza wadau pindi taarifa hizo zitakapotufikia. Kama mdau una taarifa
yoyote karibu utujuze.
Karibu kwenye blog hii ya ulimwengu wa Alizeti. Blog hii inahusu taarifa mbalimbali za zao la Alizeti pamoja na maendeleo yake na mnyororo wa thamani wa bidhaa zake, ndani na nje ya nchi. Taarifa na taaluma mbalimbali za Kilimo na usindikaji wa bidhaa mbalimbali zitokanazo na mbegu za Alizeti zitawekwa hapa kwa ajili ya kuwanufaisha wadau wa zao hili. Tafadhali, furahia ulimwengu wetu na kama una taarifa yoyote ya kuchangia, unakaribishwa sana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Pamoja na kuwapongeza ASA watuambie mbegu hiyo itatoka lini?
ReplyDelete